Isaiah 44:1-6

Israeli Aliyechaguliwa


1 a“Lakini sasa sikiliza, ee Yakobo, mtumishi wangu,
Israeli, niliyemchagua.

2 bHili ndilo asemalo Bwana,
yeye aliyekuhuluku, aliyekuumba tumboni,
yeye atakayekusaidia:
Usiogope, ee Yakobo, mtumishi wangu,
Yeshuruni,
Yeshuruni hapa maana yake ni Yeye aliye mnyofu, yaani Israeli (ona pia Kum 32:15 ).
niliyekuchagua.

3 dKwa maana nitamimina maji juu ya nchi yenye kiu,
na vijito vya maji juu ya ardhi iliyokauka;
nitamimina Roho wangu juu ya watoto wako,
nayo baraka yangu juu ya wazao wako.

4 eNao watachipua kama manyasi katika shamba la majani,
kama mierezi kando ya vijito vya maji yatiririkayo.

5 fMmoja atasema, ‘Mimi ni wa Bwana’;
mwingine atajiita kwa jina la Yakobo;
vilevile mwingine ataandika juu ya mkono wake, ‘Wa Bwana,’
na kujiita kwa jina la Israeli.

Ni Bwana, Siyo Sanamu


6 g“Hili ndilo asemalo Bwana,
Mfalme wa Israeli na Mkombozi,
Bwana Mwenye Nguvu Zote:
Mimi ni wa kwanza na Mimi ni wa mwisho;
zaidi yangu hakuna Mungu.
Copyright information for SwhKC